TP Mazembe yachanua taji la klabu bingwa Afrika
Mabingwa mara tano wa taji la klabu bingwa Afrika TP Mazembe wameendlea na kampeni yao ya kusaka taji la klabu bingwa Afrika baada ya hapo jana kuirarua Difaa El Jadida ya Morocco kwa mabao 2-0.
Imechapishwa:
Kwa ushindi huo Mazembe imefikisha alama sita na kushikilia usukani wa Kundi B ambalo pia linajumuisha MC Alger na ES Setif za Algeria
Huo ni ushindi wa pili mfululizo wa Mazembe katika hatua ya makundi ya taji hilo baaada ya kupata ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya ES Setif ya Algeria katika mchezo wa kwanza.
Mabao ya Mazembe katika mchezo huo yalifungwa kipindi cha pili na Ben Malango na Abdoulaye Sissoko.
Mazembe sasa ina alama sita ikifuatiwa na MC Alger yenye alama nne wakati Jadida ina alama moja naa ES Setif inakamata mkiaa ikiwa bila alama yoyote.
Matokeo ya mechi nyingine…
KCCA ya Uganda iliwashinda maabingwa mara nane wa michuano hiyo Al Ahly ya Misri
Township Rollers ya Botswana ilifungwa mabao 4-1 na Esperance ya Tunisia
ES Setif ilifungwa bao 1-0 na MC Alger
Wydad Casablanca ambao ni mabingwa watetezi walipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya AS Togo Ports
Mbabane Swallows ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Premiero Agosto ya Angola.