Jukwaa la Michezo
Hugo Broos:Viongozi wa soka wawe na uvumilivu kwa makocha
Imechapishwa:
Cheza - 20:56
Kocha Mkuu wa zamani wa Timu ya Taifa ya Cameroon Hugo Broos amewataka viongozi wa soka barani Afrika kuwa wavumilivu kwa makocha ikiwa wanalenga kukuza mchezo huo. Aidha kocha huyo aliyeiwezesha Cameroon kutwaa taji la Afrika mapema mwaka jana nchini Gabon amesisitiza umuhimu wa kuwa na miundombinu thabiti ya mchezo wa soka ikiwemo viwanja.