Pata taarifa kuu
CHAN 2018

Morocco kutafuta ushindi wa pili michuano ya CHAN

Morocco inarejea dimbani Jumatano usiku dhidi ya Guinea katika mchuano wake wa pili, kuwania taji la CHAN kwa wachezaji wanaocheza soka katika ligi za nyumbani.

Cameroon ikimenyana na Congo Brazaville Januari 16 2018
Cameroon ikimenyana na Congo Brazaville Januari 16 2018 http://www.cafonline.com/
Matangazo ya kibiashara

Mchuano huu utachezwa katika uwanja wa Mohamed wa tano mjini Casablanca.

Wenyeji wanakwenda katika mchuano huu wa pili wa kundi A, baada ya kuanza vema kwa kuishinda Mauritania mabao 4-0 mwishoni mwa wiki iliyopita.

Guinea nayo ilianza vibaya baada ya kufungwa na Sudan mabao 2-1 na inahitaji ushindi wa leo ili kuwa katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.

Mchuano mwingine wa kundi hili ni Sudan dhidi ya Mauritania ambayo itakuwa inajaribu kutafuta ushindi wake wa kwanza katika michuano hii.

Ratiba inayosalia kundi A, Januari 21 2018:-

  • Sudan v Morocco
  • Mauritania v Guinea

Jumanne usiku, Cameroon ilianza vibaya baada ya kufungwa na Congo Brazaville bao 1-0, mechi iliyochezwa katika uwanja wa Adrar mjini Agadir.

Ushindi huo wa Congo ulikuja kupitia Junior Makiesse kupitia mkwaju wa penalti katika dakika 73 ya mchuano huo.

Congo inaongoza kundi la D kwa alama 3 huku Angola na Burkina Faso ikiwa na alama moja baada ya kutofungana katika mchuano huo.

Ratiba Januari 18 2018:- Kundi B

  • Ivory Coast v Zambia
  • Uganda v Namibia

Ratiba Januari 19 2018:- Kundi C

  • Libya v Nigeria
  • Rwanda v Equitorial Guinea

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.