Jukwaa la Michezo
Uchambuzi wa orodha ya makundi ya timu zitakazocheza AFCON mwaka 2017 kule Gabon
Imechapishwa:
Cheza - 21:03
Juma hili kwenye makala ya Jukwaa la Michezo, tunachambua orodha ya makundi ya timu zitakazoshiriki michuano ya kombe la mataifa ya Afrika, maarufu kama AFCON, michuano itakayoanza kutimua vumbi mwezi January mwaka 2017 nchini Gabon.Pia tutaangazia sakata la ndani la klabu ya Yanga ya nchini Tanzania, ambapo wanachama na uongozi wanavutana kuhusu uwekezaji gani ufanyike kwenye klabu hiyo.