Pata taarifa kuu
SOKA-CAF

Infantino ahudhuria Mkutano Mkuu wa CAF jijini Cairo

Rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA Gianni Infantino, yupo jijini Cairo nchini Misri anakohudhuria mkutano usiokuwa wa kawaida wa Shrikisho la soka barani Afrika CAF.

Rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA Gianni Infantino
Rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA Gianni Infantino FIFA.COM
Matangazo ya kibiashara

Mkutano huu unaongozwa na Issa Hayatou rais wa CAF, pamoja na viongozi mbalimbali wa soka barani Afrika.

Ajenda kuu ya mkutano huu ni kuwachagua watu wawili watakao keti katika Baraza kuu la FIFA.

Ongezeko la watu hao wawili litafikisha idadi ya uwakilishi wa bara Afrika katika Baraza hilo kufikia wajumbe saba kutoka watano.

Wanaowania nafasi hizo mbili ni pamoja ni pamoja na Ahmad (Madagascar), Almamy Kabele Camara (Guinea), Djibrilla Hima Hamidou (Niger), Kwesi Nyantakyi (Ghana) na  Augustin Senghor (Senegal).

CAF imekuwa ikiwakilishwa katika Baraza hilo la FIFA na Issa Hayatou, Lydia Nsekera kutoka Burundi, Tarek Bouchamaoui kutoka Tunisia, Constant Omari kutoka DRC na Fatma Samoura kutoka Senegal ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.