Jukwaa la Michezo
Kenya yapata medali ya kwanza ya dhahabu katika mbio za Marathon kwa wanawake
Imechapishwa:
Cheza - 21:45
Mwanariadha Jemima Sumgong kutoka nchini Kenya, aliishindia nchi yake medali ya kwanza ya dhahabu katika historia ya mbio za Marathon katika Michezo ya Olimpiki kwa upande wa wanawake.Sumgong alimaliza mbio hizo kwa muda wa saa 2 dakika 24 na sekunde 04, akifuatwa na Eunice Jepkirui Kirwa raia wa Bahrain, ambaye alibadilisha uraia wake kutoka nchini Kenya mwaka 2013.Tunajadili hili na mengine mengi yanayoendelea nchini Brazil.