Pata taarifa kuu
TENESI-WIMBLEDON

Kerber na Serena kukutana fainali ya michuano ya Wimbledon

Bingwa mara sita, Mmarekani Serena Williams, amefanikiwa kutinga kwa mara ya tisa kucheza fainali ya michuano ya Tenesi ya Wimbledon, akiweka historia ya aina yake, na sasa atakutana na Mjerumani Angelique Kerber aliyemfunga dada yake, Venus Williams, aliyekuwa akilenga kuwa mchezaji mwanamke mkongwe kushinda taji hilo katika kipindi cha miaka 22.

Mchezaji tenesi raia wa Marekani, Serena Williams akimpongeza Elena Vesnina baada ya kumshinda kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano ya Wimbledon, 7 Julai, 2016
Mchezaji tenesi raia wa Marekani, Serena Williams akimpongeza Elena Vesnina baada ya kumshinda kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano ya Wimbledon, 7 Julai, 2016 REUTERS/Justin Tallis/Pool
Matangazo ya kibiashara

Serena ambaye anawania taji lake la saba la michuano ya Wimbledon na kulenga kupata taji lake kubwa la 22, ilimchukua dakika 48 pekee na sekunde 34, ikiwa ni nusu fainali ya kwanza iliyomalizika katika muda mfupi, baada ya kushinda kwa seti mbili bila kwa matokeo ya 6-2 na 6-0 dhidi ya Elena Vesnina anayeshika nafasi ya 50.

Matumaini ya Serena kucheza fainali za mwaka huu dhidi ya dada yake kwa mara ya tano na mara ya tisa katika michuano mikubwa, yalizimwa wakati mchezaji nambari nne kwa ubora wa mchezo huo, Angelique Kerber, bingwa wa michuano ya Australian Open, kwa kumfunga kwa seti mbili bila kwa matokeo ya 6-4 na 6-4.

Angelique Kerber, mchezaji tenesi raia wa Ujerumani, akimpongeza Venus Williams baada ya kumfunga kwenye mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Wimbledon, Juali 7, 2016
Angelique Kerber, mchezaji tenesi raia wa Ujerumani, akimpongeza Venus Williams baada ya kumfunga kwenye mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Wimbledon, Juali 7, 2016 REUTERS/Gerry Penny/Pool

Serena ambaye alikuwa anacheza mchezo wake wa 32 kwenye michuano mikubwa ya Tenesi, alimsambaratisha Vesnina na kisha kubusu uwanja mbele ya mwanamfalme wa Uingereza, Williams.

Fainali ya michuano hiyo sasa itamkutanisha Angelique Kerber na Serena Williams, ambao walicheza kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano ya US Open.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.