Pata taarifa kuu
CHAN 2016-ZAMBIA-MALI

CHAN 2016: Zambia na Mali zatoka sare ya kutofungana

Timu ya Mali itachuana na ile ya Tunisia katika robo fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika, Januari 31 mjini Kigali. Mali imehakikisha kufuzu kwake kufuatia sare ya 0-0 dhidi ya Zambia, Jumatano hii 27 Januari.

Mchezaji wa Mali Sekou Koita.
Mchezaji wa Mali Sekou Koita. Courtesy of cafonline
Matangazo ya kibiashara

Mali na Zambia ni miongoni mwa timu zinazounda kundi D katika michuano ya CHAN 2016. Zambia watapepetana na Guinea siku ya Jumapili katika uwanja wa mpira wa Rubavu.

Zambia-Mali hayatakumbukwa. Mbali na mbili nzuri na mbali shots juu ya lengo, beki saini Dieng Aliou (28) na Lassana Samake mazingira (35), si gani kuweka katika vinywa vyao, katika kipindi cha kwanza, Januari 27 mjini Kigali.

Sare hii imepelekea Zambia kuchukua nafasi ya pili, huku nafasi ya kwanza ikichukuliwa na Mali.

Mikwaju ya mbali ya iliyoelekezwa langani ya beki Aliou Dieng katika dakika ya 28na kiungo wa kati Lassana Samake katika dakika ya 35 haikuzaa matunda yoyote katika kipindi cha kwanza cha mchuano wa Jumatano hii Januari 27.

Zambia tayari imefuzu na imechukua nafasi ya pili katika kundi D.

Zimbabwe yajiinulia heshima katika mechi nyingine

Katika mchuano kati ya Zimbabwe na Uganda, Zimbabwe imefuzu robo fainali kwa kuibwaga Uganda bao bao 1-0, bao lililofungwa na Manondo katika dakika ya 50 ya mchezo. Uganda imeaga michuano ya CHAN 2016.

Timu za kundi D jinsi zinavyoshindana

1. Zambia pointi 7 - imefuzu
2. Mali pointi 5 - imefuzu
3. Zimbabwe pointi 3 - imebanduliwa
4. Uganda pointi 1 - imebanduliwa

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.