Jukwaa la Michezo
Uchambuzi wa matukio ya michezo yaliyojiri juma nzima barani Afrika
Imechapishwa:
Cheza - 20:30
Juma hili katika Jukwaa la Michezo, tunaangazia hatua ya Shirikisho la soka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuachana na harakati za kutaka kuwa wenyeji wa michuano ya soka baina ya mataifa ya Afrika mwaka 2019, lakini pia tunachambua hatua ya Shirikisho la soka barani Afrika CAF, kumfungia kocha wa timu ya taifa ya soka ya Kenya Adel Amrouche miezi 12 kwa kumtemea mate afisaa wa CAF mwezi Juni nchini Comoros.Ungana na Victor Abuso, Emmanuel Makundi, Collins Libert Adede na Kahozi Kosha kupata uchambuzi wa kina.