Pata taarifa kuu
MAREKANI-IS-MASHARIKI YA KATI-USALAMA

Mike Pompeo: Marekani itaendelea na vita dhidi ya Islamic State

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo amesema nchi yake itahakikisha kuwa kundi la Islamic State halipati nafasi ya kujikusanya tena na kurejea kwenye ukanda wa Mashariki ya Kati.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo. Reuters/路透社
Matangazo ya kibiashara

Matamshi ya Pompeo ameyatoa wakati huu akianza ziara katika mataifa ya kiarabu kuyapa hakikisho kuwa nchi yake itaendelea na vita dhidi ya kundi hilo licha ya kutangaza mpango wa kuanza kuwaondoa wanajeshi wake nchini Syria.

Ziara ya Pompeo inakuja wakati huu maofisa kadhaa wa juu katika wizara ya ulinzi ya Marekani wakitangaza kujiuzulu nafasi zao, majuma kadhaa baada ya rais Donald Trump kutangaza kuwaondoa wanajeshi wake nchini Syria akisema kundi la Islamic State limedhibitiwa.

Pompeo anatembelea nchi za kiarabu ikiwa ni siku chache tu tangu mshauri wa masuala ya usalama wa taifa wa Marekani John Bolton, afanye ziara nchini Israel na Uturuki kuwahakikishia nchi washirika kuwa vita dhidi ya Islamic State itaendelea.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.