Umoja wa Mataifa waendelea na jitihada zake za kuepo kwa mazungumzo Yemen
Ndege ya Umoja wa Mataifa imewasafirisha wapiganaji wa Kihouthi kutoka nchini Yemen, kama jitihada za kujenga uaminifu wa kuwepo kwa mazungumzo ya amani kati ya waasi hao na serikali.
Imechapishwa:
Hili limethibutishwa na jeshi la Saudi Arabia, linaloongoza operesheni dhidi ya waasi hao.
Waasi hao wanasafirishwa kwenda jijini Sanaa, na baadaye nchini Oman kupata matibabu zaidi.
Saudi Arabia na washirika wake wamekuwa wakishtumiwa kwa ukiukwai wa haki za binadamu katika vita vinvyoendelea nchi Yemen katika ya jeshi la serikali linaloungwamono na Saudi Rabaia na waasi wa Kihouthi wanaoungwa mkono na Iran.
Machafuko nchini Yemen yamesababisha vifo vya watu wengi na mamia kwa maelfu kulazimika kuyahama makazi yao.