Pata taarifa kuu
SYRIA-MAZUNGUMZO-AMANI

Upinzani nchini Syria wakataa mazungumzo ya amani yaliyopangwa na Urusi

Muungano wa upinzani nchini Syria umesema hautashiriki katika mazungumzo ya amani yaliyoandaliwa na Urusi.

Mashambulizi ya hivi karibuni nchini Syria, wanajeshi wa Uturuki wakishambulia ngome za wapiganaji wa Kikurdi
Mashambulizi ya hivi karibuni nchini Syria, wanajeshi wa Uturuki wakishambulia ngome za wapiganaji wa Kikurdi BULENT KILIC / AFP
Matangazo ya kibiashara

Hili ni pigo kwa serikali ya Urusi ambayo imekuwa ikijaribu kuwashawishi wapinzani kuja kwenye meza ya mazungumzo.

Mazungumzo hayo yalikuwa yamepangwa kufanyika wiki ijayo mjini Sochi, yakiongozwa na Urusi ambayo imekuwa ikiisaidia serikali ya rais Bashar Al Assad kupambana na waasi.

Upinzani nchini Syria umesema, baada ya mashauriano ya kina pamoja na wawakilishi wa Umoja wa Mataifa na nchi nyingine, hawajaridhishwa na hatima ya mazungumzo hayo.

Makundi mengine ya waasi ambayo yapo kwenye upinzani nchini Syria nayo yamekataa kushiriki katika mazungumzo hayo.

Mbali na mazungumzo haya yaliyokuwa yamepangwa na Urusi, Umoja wa Mataifa umekuwa ukijaribu pia kupatanisha pande zote mbili bila mafanikio.

Siku ya Ijumaa, msuluhishi wa mzozo huu Staffan de Mistura alishindwa kuafikiana na wawakilishi wa serikali na upinzani, katika mazungumzo mengine yaliyokuwa yanaendelea mjini Vienna nchini Austria.

Mzozo nchini Syria umeendelea kwa mwaka wa saba sasa na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 300,000 na mamilioni kuyakimbia makwao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.