Pata taarifa kuu
SYRIA-MAZUNGUMZO-SIASA

Upinzani Syria wataka Marekani kuingilia kati mazungumzo

Upinzani nchini Syria, inasema itazungumza na Marekani ili kuingilia kati mazungumzo ya amani yanaoongozwa na Umoja wa Ulaya.

Ujumbe wa upinzani nchini Syria ukiwa katika mazungumzo ya amani Geneva Aprili 18, 2015.
Ujumbe wa upinzani nchini Syria ukiwa katika mazungumzo ya amani Geneva Aprili 18, 2015. REUTERS/Denis Balibouse
Matangazo ya kibiashara

Mjumbe wa upinzani katika mazungumzo hayo amesema, upinzani hautaki Urusi kuonekana kuwa mstari wa mbele kuongoza mazungumzo hayo.

Wito huu wa upinzani unakuja kuelekea mazungumzo mapya, yanayotarajiwa kuanza tarehe 21 mwezi huu jijini Genva nchini Uswisi.

Hadi sasa mazungumzo yote yaliyofanyika, hayajazaa matunda.

Mchafuko nchi Syria yamesababisha maelfu ya watu kuuawa na wengine kuyahama makazi yao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.