Pata taarifa kuu
URUSI-MAREKANI-SYRIA-USALAMA

Urusi yaishutumu Marekani kutoa mafunzo kwa wapiganaji wa zamani wa IS

Mkuu wa majeshi ya Urusi ameishtumu Marekani kutoa mafunzo kwa wapiganaji wa zamani wa kundi la Islamic (IS) nchini Syria ili kuhatarisha usalama wa nchi hiyo

Marekani inasisitiza kuwa kambi ya Tanf ni kambi ya muda mfupi inayotumiwa kutoa mafunzo kwa vikosi vinavyotoa ushiriki wao kwa kupambana na wapiganaji wa IS.
Marekani inasisitiza kuwa kambi ya Tanf ni kambi ya muda mfupi inayotumiwa kutoa mafunzo kwa vikosi vinavyotoa ushiriki wao kwa kupambana na wapiganaji wa IS. REUTERS/Erik De Castro
Matangazo ya kibiashara

Jenerali Valery Guerassimov amesema, katika mahojiano yaliyochapishwa na gazeti la kila siku la Komsomolskaya Pravda, kwamba jeshi la Marekani linatumia kambi ya kijeshi ya Tanf, kambi kubwa kwa mawasiliano muhimu kwenye mpaka wa Iraq kusini mwa Syria.

Kambi hii iliotajwa kinyume cha sheria na eneo lilinaloizunguka vinaunda "shimo nyeusi" ambalo wapiganaji wa Kiiislamu wanaweza kuendesha mazoezi yao,Jenerali Guerassimov amebaini.

Marekani inasisitiza kuwa kambi ya Tanf ni kambi ya muda mfupi inayotumiwa kutoa mafunzo kwa vikosi vinavyotoa ushiriki wao kwa kupambana na wapiganaji wa IS.

Jeshi la Marekani limekanusha mara kadha tuhuma hizo dhidi yake.

Jenerali Guerassimov amesema kuwa wapiganaji hao wa zamani wa IS wanajiita Jeshi Jipya la Syria au wanatumia majina mengine.

Uwepo wa wapiganaji hawa katika kambi ya Tanf uligunduliwa na satelaiti pamoja na ndege zisizokuwa na rubani za Urusi. Jenerali Guerassimov ameongeza kuwa sehemu kubwa ya wanajihadi na askari wa zamani wa IS pia wako katika mji wa Chadadi,katika kambi nyingine ya Marekani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.