Pata taarifa kuu
SYRIA-URUSI-USALAMA

Putin agiza sehemu moja ya askari wake kuondoka Syria

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameamuru kuondolewa kwa sehemu ya kikosi cha wanajeshi wa nchi yake ambao wamekuwa wakipambana na waasi nchini Syria.

Rais wa Urusi Vladimir Putin (2wa pili kushoto, mbele), Waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu (kushoto, mbele) na Rais wa Syria Bashar al-Assad (wa pili kulia, mbele) wakitembelea kambi ya kikosi cha angani cha Hmeymim katika Mkoa wa Latakia, Syria Desemba 11.
Rais wa Urusi Vladimir Putin (2wa pili kushoto, mbele), Waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu (kushoto, mbele) na Rais wa Syria Bashar al-Assad (wa pili kulia, mbele) wakitembelea kambi ya kikosi cha angani cha Hmeymim katika Mkoa wa Latakia, Syria Desemba 11. Sputnik/Mikhail Klimentyev/Sputnik via REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Putin ametoa agizo hilo baada ya ziara yake ya kushtukiza nchini Syria katika jimbo la Latakia, alikopokelewa na rais Bashar al-Assad.

Hatua hii imekuja baada ya Urusi hivi karibuni kusema kuwa, ilikuwa imemaliza kazi yake nchini Syria baada ya kulemewa kwa wapiganaji wa Islamic State.

Rais Bashar, alikuwa nchini Urusi hivi karibuni na kumshukuru rais Putin kwa kulisaidia taifa lake.

Jeshi la Urusi limekuwa nchini Syria tangu mwaka 2015, baada ya kuombwa na serikali ya Damascus kusaidia katika makabiliano na waasi wanaopinga serikali ya rais Assad.

Zaidi ya watu 340,000 wameuwawa nchini Syria tangu mwezi Machi mwaka 2011 ulipoibuka mgogoro, uliopelekea serikali kupambana na makundi ya kigaidi pamoja na ya waasi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.