Ndege ya kivita yauwa watu 30 nchini Syria
Mashirika ya kutetea haki za binadmau nchini Syria yanasema, shambulizi la angaa limesababisha vifo vya watu 30 Mashariki mwa nchi hiyo.
Imechapishwa:
Ripoti zinasema kuwa shambulizi hilo limetokea katika eneo la al-Dablan.
Haijafahamika wamiliki wa ndege iliyotekeleza shambulizi hilo kwa mujibu wa ripoti ya muungano wa mashirika hayo ya kutetea haki za binadamu.
Muungano wa mataifa yanayoshirikiana na Marekani pamoja na zile za Urusi, zimekuwa zikishambulia kundi la Islamic State nchini Syria.
Siku ya Jumatatu, shambulizi kama hili lilitekelezwa katika eneo la al-Mayadeen na kusababisha vifo vya watu 57.
Hakuna aliyejitokeza na kudai kutekeleza shambulizi hili la siku ya Jumatano.