Pata taarifa kuu
SYRIA-GENEVA-UN

Upinzani wa Syria waituhumu Serikali kutaka kukwamisha mazungumzo yanayoendelea

Muungano wa upinzani wa Syria unaoshiriki kwenye mazungumzo ya kusaka suluhu mjini Geneva, wanautuhumu utawala wa Damascus kwa makusudi kujaribu kukwamisha mazungumzo yanayoendelea, baada ya mpatanishi mkuu wa mzozo huo kuzitaka pande zote kujiepusha na mashambilizi zaidi, ambapo amelaani shambilio la mwishoni mwa juma kwenye mji wa Homs.

Kiongozi wa ujumbe wa upinzani kwenye mazungumzo ya Syria yanayofanyika mjini Geneva, Nasr al-Hariri
Kiongozi wa ujumbe wa upinzani kwenye mazungumzo ya Syria yanayofanyika mjini Geneva, Nasr al-Hariri REUTERS/Pierre Albouy
Matangazo ya kibiashara

Kamati ya juu ya majadiliano ya upinzani, imetoa kauli hiyo baada ya mwakilishi wa Serikali balozi Bashar al-Jaafari kusema kuwa ikiwa mpinzani yeyote hatalaani shambulio la kwenye mji wa Homs, watawahesabu kama magaidi.

Upinzani huo unasema kuwa, utawala wa Syria kwa makusudi kabisa hataki nchi hiyo ipate suluhu ya kisiasa na kwamba balozi Jaafari anajaribu kupindisha kile kilichowapeleka mjini Geneva.

Wapinzani wanasema toka kwenye mazungumzo ya awali yaliyofanyika mjini Geneva, neno pekee ambalo utawala wa Damascus unalijua ni "ugaidi".

Kiongozi wa ujumbe wa Serikali ya Syria kwenye mazungumzo ya amani yanayoendelea mjini Geneva, Bashar al-Jaafari
Kiongozi wa ujumbe wa Serikali ya Syria kwenye mazungumzo ya amani yanayoendelea mjini Geneva, Bashar al-Jaafari REUTERS/Pierre Albouy

Mjumbe maalumu wa umoja wa Mataifa, Staffan de Mistura alianzisha mazungumzo mengine ya raundi ya nne mjini Geneva alhamisi ya wiki iliyopita, na kama ilivyoshuhudiwa kwenye mikutano iliyopita ni wazi kumekuwa na hatua ndogo sana ambazo zimepigwa kwenye mazungumzo haya.

Shambulio la kwenye mji wa Homs mwishoni mwa juma, lililenga vituo viwili vya kijeshi, ambapo mamia ya watu waliuawa akiwemo mkuu wa intelijensia wa vikosi vya rais Assad.

Ujumbe wa Serikali unaoshiriki mazungumzo mjini Geneva, umepa kutofumbia macho shambulio la mwishoni mwa juma na kuapa kulipa kisasi, hali ambayo tayari imeanza kushuhudiwa kwa vikosi vya Serikali kutekeleza mashambulizi ya anga mfululizo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.