Mmoja wa viongozi wa Taliban kaskazini mwa Afghanistan auawa
Kiongozi wa Taliban katika mkoa wa Kunduz kaskazini mwa Afghanistan ameuawa. Kifo chake kimethibitishwa na kundi la Taliban. Kiongozi huyo aliuawa na ndege isio na rubani. Alikua mmoja wa wapiganaji wa Taliban walioteka kwa muda kwa mara ya kwanza mji wa Kunduz mwaka 2015.
Imechapishwa:
Hii si mara ya kwanza kifo cha Abdul Salam Akhund kutangaza. Lakini wakati huu taarifa imethibitishwa na Msemaji wa kundi la Taliban. Msemaji wa Taliban anasema kuwa Abdul Salim aliuawa Jumapili kwa makombora yaliyorushwa na ndege isio na rubani ya Marekani wakati ambapo alikua wilayani Archi kaskazini mwa mkoa wa Kunduz.
Shambulizi hilo limethibitishwa na jeshi la Marekani, ambalo halijasungumzia idadi ya waliouawa katyika shambulizi hilo. Hata hivyo viongozi wa serikali za mitaa wamearifu kwamba, wapiganaji tisa wa Taliban waliuawa wakati wa operesheni hiyo.
Aidha, ripoti zinasema kuwa pamoja na Kamanda huyo, wapiganaji wengine watatu wa kundi hilo wameuawa baada ya kushambuliwa.