Pata taarifa kuu
ISRAEL-GAZA-USALAMA

Israel yaendesha mashambulizi katika Ukanda wa Gaza

Ndege za kijeshi za Israel ziliendesha mashambulizi Jumatatu hii katika Ukanda wa Gaza na kusababisha watu wanne kujeruhiwa. serijkali ya Israel inasema imechukua uamuzi wa kuendesha mashambulizi hayo baada ya kitendo cha watu wasiojulikana kurusha roketi kusini mwa Israel.

Ukanda wa Gaza wakabiliwa na mashambulizi ya ndege za kivita za Israel.
Ukanda wa Gaza wakabiliwa na mashambulizi ya ndege za kivita za Israel. AFP PHOTO / THOMAS COEX
Matangazo ya kibiashara

Jeshi la Israel linasema lililenga ngome tano za kundi la Hamas, kundi la Kiislamu linalodhibiti ardhi ya Palestina kwa karibu miaka kumi.

Kwa mujibu wa serikali ya Israel, roketi ilianguka katika eneo lisilokua na watu na haikusababisha hasara yoyote.

Hakuna kundi ambalo limedai kuhusika na kitendo hicho, lakini serikali ya Israel inalinyooshea kidole cha lawama kundi la Hamas linahusika kwqa kuzorotesha usalama katika eneo linalodhibiti tangu Juni 2007.

Kundi hili la Kiislamu lilisitisha mapigano kimyakimya tangu mashambulizi ya Israel mwaka2014, lakini kuna baadhi ya wanajihadi kutoka kundi hilo ambao mara kwa mara wamekua wakirusha roket nchini Israel.

Waziri wa Ulinzi wa Israel Avigdor Lieberman amesema Israel "haikua na nia yoyote ya kushiriki katika operesheni yoyote ya kijeshi katika Ukanda wa Gaza, lakini haitovumilia kitendo cha kurusha roketi katika baadhi ya maeneo yake".

Fawzi Barhoum, Msemaji wa Hamas, amesema Israel itahusika na kuongezeka ka machafuko kama itaendelea kulenga "ngome za Hamas".

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.