Pata taarifa kuu
SYRIA-IS

Islamic State yatimuliwa katika mji wa Dabiq

Waasi wa Syria wanaoungwa mkono na Uturuki wameuteka Jumapili hii Oktoba 16 mji wa Dabiq, mji ulio karibu na mpaka wa Uturuki, ambao mpaka sasa ulikua moja ya ngome kuu ya kundi la Islamic State kaskazini mwa jimbo la Aleppo.

Wapiganaji wa kundi a waasi la Free Syrian Army (FSA), wakipambana dhidi ya kundi la Islamic State katika mji wa Dabiq, Oktoba 15, 2016.
Wapiganaji wa kundi a waasi la Free Syrian Army (FSA), wakipambana dhidi ya kundi la Islamic State katika mji wa Dabiq, Oktoba 15, 2016. Nazeer al-Khatib / AFP
Matangazo ya kibiashara

Mwezi Agosti 2014, waasi hao walijikuta mji wao ukianguka mikononi mwa kundi la Islamic State. Jumapili hii, wakazi wa mji wa Dabiq wamesema kufurahishwa na kutimuliwa kwa kundi la Islamic State katika mji wao. Kwa sasa kwa kuwa wanajihadi wametimuliwa kabisa katika mji huo, shughuli za kukagua na kutegua mabomu yaliyotegwa ardhini zinaendelea.

Shirika la Haki za Binadamu nchini Syria, limebaini kwamba 'waasi waliudhibiti mji wa Dabiq baada ya kuondoka kwa wapiganaji wa kundi la IS'. Moja ya makundi ya waasi limeeleza kwamba mapigano yalikua makali. Waasi tisa waliuawa wakati wa mapigano hayo. Makundi mengine ya waasi yamebaini kwamba upinzani wa kundi la IS ulikuwa 'mdogo'.

Kulingana na imani ya Waislam wenye msimamo mkali, vita vya mwisho kati ya jeshi la Waislam na makafiri vitatokea katika mji huu na itakuwa mwanzo wa Kiyama. Ushahidi muhimu wa mji huu kwa wanajihadi, kundi la Islamic State lililipa gazeti lake kuu jina la mji huu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.