IRAQ-IS
Iraq yaanzisha operesheni dhidi ya IS Falluja
Waziri Mkuu wa Iraq, Haider al-Abadi ametangaza kuanza operesheni ya kijeshi kuuchukua mji wa Falluja kutoka kwa kundi la Islamic State.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Jeshi limetoa wito kwa raia wanaoishi katika mji huo kuanza kuondoka kabla ya kuanza kwa mashambulizi hayo.
Hata hivyo, wakazi ambao hawataweza kuondoka wameshauriwa kusimika bendera nyeupe juu ya nyumba zao ili kutambuliwa na jeshi.
Mji wa Falluja ulikuwa wa kwanza, kudhibitiwa na kundi la Islamic State mwaka 2014 na ndio mji unaosalia mikononi mwa magaidi.