Mkutano kuhusu masuala ya idadi ya watu na maendeleo kuanza Jumanne Nairobi
Maelfu ya wajumbe kutoka mataifa mbalimbali duniani wapo jijini Nairobi nchini Kenya, kuhudhuria mkutano wa siku tatu, unaoanza Jumanne wiki hii kujadili masuala ya idadi ya watu na maendeleo.
Imechapishwa:
Idadi kubwa ya wajumbe hao ni vijana, lakini pia mkutano huo unatarajiwa kugusia masuala yanayowaathiri vijana hasa afya, mapenzi na suala la upangaji uzazi.
Viongozi wa Kanisa Katoliki wameshtumu hatua ya Kenya kukubali kuwa mwenyeji wa mkutano huo na kusema kuwa Kanisa hilo halitahudhuria mkutano huo.
Rais wa muungano wa mashirika ya kiraia nchini Kenya Suba Churchil, amesema baadhi ya watu hawajaelewa kiini cha mkutano huo.
Wadadisi wanasema idadi ya watu barani Afrika inakuwa kwa kasi ambapo kufikia mwaka 2050 itakuwa imeongezeka maradufu ya ilivyo sasa, huku 40% ya watu masikini kabisa duniani wakihofiwa kuja kuishi kwenye mataifa mawili tu ya bara hilo.