Pata taarifa kuu
TANZANIA-MAJANGA ASILI-TABIA NCHI

Mvua zasababisha baadhi ya shughuli kukwama Dar es Salaam

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchiniTanzania (MET) imetoa tahadhari juu ya kuwepo kwa mvua kubwa ambayo itaupiga ukanda wa pwani wa nchi hiyo kwa siku tatu mfululizo kutokea leo Jumatatu Mei 13 mpaka Jumatano Mei 15.

Athari ya mafuriko katika jiji la Dar es salaam nchini Tanzania April 16 2018. (Picha ya zamani)
Athari ya mafuriko katika jiji la Dar es salaam nchini Tanzania April 16 2018. (Picha ya zamani) http://www.mwananchi.co.tz/
Matangazo ya kibiashara

MET pia imetahadharisha kuwa kwa siku za Alhamisi na Ijumaa wiki hii, ukanda huo wa pwani ya Tanzania utakabiliwa na upepo mkali.

Mvua inayoendelea kunyesha imeathiri huduma ya usafiri wa umma hasa usafiri wa mwendokasi, katika mji mkuu wa Tanzania, Dar es Salaam.

Kampuni ya Mabasi ya mwendo kasi (Udart) imelazimika kusitisha huduma zake za usafiri kwa mabasi yanayotumia barabara kuu ya Morogoro, eneo la Jangwani na barabara ya Kawawa katika Bonde la Mkwajuni kuelekea Morocco.

Taarifa ya Mkuu wa Idara ya Mawasiliano ya Udart, Deus Bugaywa imeeleza kuwa safari zilizositishwa ni kati ya Kimara -Kivukoni, Kimara - Gerezani, Morocco - Kivukoni na Morocco -Gerezani kuanzia mapema alfajiri ya leo Jumatatu.

Wakaazi wa maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam wamekubwa na adha kubwa ya foleni kutokana na mvua hizo kuharibu ama kuziba baadhi ya barabara muhimu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.