Dunia yaadhimisha miaka 70 ya mkataba wa haki za binadamu huku Afrika mashariki, haki za binadamu zikipitia changamoto
Disemba 10 kila mwaka dunia huadhimisha siku ya haki za binadamu, tukio linalokumbukwa baada ya kutiwa saini kwa azimio la haki za binadamu mwaka 1948.
Imechapishwa:
Cheza - 02:19
Wakati dunia ikiadhimisha siku hii muhimu, mataifa ya Afrika Mashariki yanapitia changamoto mbalimbali za ulinzi wa haki za binadamu ikiwemo mauaji, utekaji nyara wa wanaharakati na waandishi wa habari, utekaji, ukeketaji na vitendo vya uhalifu.
Hata hivyo mataifa ya Afrika Mashariki yanapiga hatua katika utoaji wa huduma za kijamii ikiwemo elimu.
Mwandishi wetu Fredrick Nwaka ameandaa ripoti hii baada ya kuhudhuria adhimisho la siku hii jijini Dar es Salaam nchini Tanzania.