Pata taarifa kuu
TANZANIA-UVUVI-BIASHARA

Biashara ya samaki yadorora katika soko la Kimataifa la Ferry Jijini Dar es Salaam

Wafanyabiashara wa samaki katika soko la samaki la Kimataifa la Ferry Jijini Dar es Salaam wameelezea kusuasua kwa biashara zao siku chache baada ya kuripotiwa mabadiliko ya hali ya hewa na viuashiria vya mvua.

Picha ikionyesha uhaba wa samaki katika soko la Feri Jijini Dar es salaam Oktoba 26, 2018
Picha ikionyesha uhaba wa samaki katika soko la Feri Jijini Dar es salaam Oktoba 26, 2018 RFI/ Fredrick Nwaka
Matangazo ya kibiashara

Mwandishi wetu Fredrick Nwaka mapema leo alifika sokoni hapo na kuzungumza na wachuuzi na watumiaji wa kitoweo hicho ambao wengi wamekiri bei ya kitoweo hicho imeongezeka maradufu.

"Bei ya samaki imeongezeka sana, jambo linalotupatia wakati mgumu sisi wachuuzi kukuza biashara zetu,"alieleza mchuuzo mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Seif Hamis

Ufukwe ulio pembezoni mwa soko la samaki la Ferry ukionyesha wachuuzi na watumiaji wa kitoweo cha samaki
Ufukwe ulio pembezoni mwa soko la samaki la Ferry ukionyesha wachuuzi na watumiaji wa kitoweo cha samaki RFI/Fredrick Nwaka

Soko la samaki la Ferry hutegemewa na wafanyabiashara wengi katika Jiji la Dar es salaam na hata nje ya nchi. Mara kadhaa serikali ya Tanzania imechukua hatua za kuhakikisha soko hilo linakidhi viwango vya kimataifa kwa kuhudimia wakazi wa ndani na nje ya nchi.

Mapema wiki hii, Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania, TMA ilitoa tangazo ikionya wavuvi kutoingia baharini kutokana na upepo mkali.

Ni kilio cha hali ngumu ya biashara katika soko la kimataifa la samaki la Ferry Jijini Dar es Salaam. Hapa wachuuzi wa samaki wanapiga moyo konde licha ya hali ngumu ya biashara.

Soko la samaki la kimataifa la Ferry, wachuuzi wakihaha kusaka kitoweo cha samaki
Soko la samaki la kimataifa la Ferry, wachuuzi wakihaha kusaka kitoweo cha samaki RFI/Fredrick Nwaka

Mwajuma yo ni Ofisa Uvuvi na Kaimu Mwenyekiti wa Soko la Samaki la Ferry amesema licha ya hali ya kibiashara kuwa tete lakini usalama ni suala la muhimu kwa watumiaji wote wa soko hilo wakiwemo wavuvi.

Fuatilia matangazo yetu ya jioni saa 12 Jioni ili kupata undani wa taarifa hii na nyinginezo

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.