Habari RFI-Ki
Wanasiasa Burundi watofautiana kuhusu uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Uchaguzi
Imechapishwa:
Cheza - 08:51
Wanasiasa nchini Burundi wametofautiana kuhusu uteuzi wa wajumbe saba wapya walioteuliwa katika Tume ya Uchaguzi CENI. Wanasiasa wa upinzani wakiongozwa na Agathon Rwasa anayeongoza chama cha FNL ,wanasema wajumbe hao wapya ni vibaraka wa chama tawala. Makamu wa kwanza wa rais Gaston Sindimwo naye anasema hakushirikishwa. Je, hii inamaanisha nini ?