Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda aanika vipaumbele vyake, akiwania uongozi La Francophone
Waziri wa mambo ya nje wa Rwnada Louise Mushikiwabo ameweka wzi vipaumbele vinne atakavyovyifanyia kazi endapo atachaguliwa kuwa katibu mkuu muungano wa nchi zinazozungumza lugha ya kifaransa Duniani, La Francophone.
Imechapishwa:
Akitumia ukurasa wake wa Twitter, Mushikiwabo ametaja vipaumbele hivyo kuwa ni ajira, kuongeza ushawishi wa lugha ya kifaransa duniani, kubadilishana uzoefu na ya mataifa yanayozungumza lugha ya kifaransa duniani.
Kiongozi huyo, amesema vipaumbele vyake vinalenga kutafuta suluhu ya changamoto za pamoja zinazozikabili nchi wanachama wa La Francophone.
Katika uchaguzi huo, Mushikiwabo atachuana na Michaelle Jean raia wa Canada aliyezaliwa nchini haiti.
Jumuiya hiyo yenye nchi 84 inatarajiwa kufanya uchaguzi wake Oktoba 11 na 12, uchaguzi utakaofanyika nchini Armenia.