Habari RFI-Ki
Kenya yapeleka vita vya ufisadi nje ya mipaka ya nchi yake
Imechapishwa:
Cheza - 10:00
Kenya imepeleka vita dhidi ya ufisadi nje ya mipaka ya nchi hiyo, baada ya kutia saini mkataba na serikali ya Uswisi, ili kusaidia kurejeshwa nyumbani Mabilioni ya Dola, fedha za umma, zilizoibiwa na watu mbalimbali na kufichwa katika Benki za Uswisi.Mkataba kama huu pia, hivi karibuni ulisainiwa nchini Nigeria na kuisaidia nchini hiyo kupata Dola Bilioni 1.2, fedha za umma zilizokuwa zimeibiwa.Unafikiri njia hii inasaidia vipi mafanikio ya kupambana na ufisadi kwa mataifa ya Afrika ?