Pata taarifa kuu
KENYA-UFISADI-UCHUMI

Kenya imeanza kuwakamata viongozi wanaojihusisha na ufisadi

Vita dhidi ya ufisadi nchini Kenya, vinaendelea kushika kasi baada ya kukamatwa na kuzuiwa kwa Gavana wa Kaunti ya Busia Sospeter Ojamong. Mahakama inatarajia kutoa uamuzi Ijumaa wiki hii iwapo itampa dhamana au la.

Maofisa wa polisi wa Kenya wakiwa mbele ya Mahakama Kuu, huku mvua ikinyesha, Nairobi, Kenya, Novemba 14, 2017.
Maofisa wa polisi wa Kenya wakiwa mbele ya Mahakama Kuu, huku mvua ikinyesha, Nairobi, Kenya, Novemba 14, 2017. AP
Matangazo ya kibiashara

Gavana wa jimbo la Busia, magharinbi mwa Kenya Sospeter Ojamoong amekuwa kiongozi wa kwanza wa haiba kuzuiliwa na mahakama ya nchi hiyo kwa tuhuma za ufisadi na matumizi mabaya ya afisi , kati ya magavana wanne ambao Tume ya Kukabiliana naUfisadi ilitangaza kuwachunguza dhidi ya madai ya ufisadi.

Jumatano wiki hii Bw Ojamoong, alitiwa mbaroni na maafisa wa Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi na kuhojiwa kuhusu ufujaji wa shilingi milioni 20 sawa na dola za Marekani 200,000 .

Bw Ojamoong ataendelea kuzuiliwa jela hadi siku ya Ijumaa wiki hii, mahakama itakapotoa uamuzi wake iwapo yeye na wenzane watatu wataachiliwa au la. Tume ya kupambana na Ufisadi imepinga kuachiliwa kwa dhamana kwa gavana huyo kwa madai kwamba huenda akahitilafiana na uchunguzi dhidi yake. Hata hivyo Ojamoonga alionekana mtulivu na mwenye imani kabla ya kuanza kwa kesi yake.

Katika kesi inayomkabili, Ojamoonga anahusishwa na mashitaka saba ya ufisadi, ikiwa ni pamoja na ufujaji wa shilingi milioni 20 katika hazina ya maendeleo ya Kaunti ya Busia sawa na matumizi mbaya ya afisi. Akitoa uamuzi wake hakimu mkuu wa mahakama ya kukabiliana na Ufisadi Douglas OgotAamesema kesi hiyo inahusisha mashitiaka tata ya maadili na inachukuliwa ya muhimu ka umma, na kubaini kwamba atatoa uamuzi wa kina siku ya Ijumaa.

Awali wanasheria wa gavana Ojamoong wakiongozwa na Seneta wa Siaya James Orengo waliomba mahakama kumuachilia kwa dhamana gavana huyo, ombi ambalo limepingwa na mwanasheria wa serikali Alexander Muteti.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.