Pata taarifa kuu
KENYA-SIASA

Sintofahamu yaendelea kujitokeza kwa wanasiasa Kenya

Kinara wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga, Jumatano wiki hii anatarajiwa kurejea nchini mwake akitokea nchini Uingereza lakini safari hii huenda asipokelewe kama ilivyozoeleka na badala yake atakutana na shinikizo kubwa la kisiasa kuhusu wito wake wa kufanyika kwa marekebisho ya katiba.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta (kushoto) na Raila Odinga, kiongozi wa chama cha upinzani (NASA), Machi 9, 2018Nairobi, Kenya.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta (kushoto) na Raila Odinga, kiongozi wa chama cha upinzani (NASA), Machi 9, 2018Nairobi, Kenya. ©SIMON MAINA/AFP
Matangazo ya kibiashara

dinga anarejea ikiwa ni siku 3 tu zimepita tangu rais Uhuru Kenyatta atupilie mbali wito wa kufanyika marekebisho ya katiba hali inayozusha maswali kuhusu makubaliano yao ya Machi 9 ikiwa yatafanikiwa.

Hata hivyo makubaliano na wito huu ni mambo yanayoonekana kumkera naibu wa rais wa Kenya, William Ruto ambaye amewakejeli wanasiasa wanaotaka kutumia mgongo wa katiba kujinufaisha.

Tangu kushikana mikono kwa rais Kenyatta na Odinga wanasiasa nchini Kenya wamegawanyika huku baadhi wakiona makubaliano haya ni njama za kumtupa kando naibu wa rais Ruto.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.