Pata taarifa kuu
KENYA-AFYA

Magavana watakiwa kukutana kwa mazungumzo na wauguzi wanaogoma

Chama cha wauguzi nchini Kenya kimeomba baraza la magavana kufikiria kufanya mazungumzo na wauguzi ambao wako kwenye mgomo kabla ya kuchukua hatua za kinidhamu.

Baadhi ya wauguzi nchini Kenya wanaendelea na mgomo.
Baadhi ya wauguzi nchini Kenya wanaendelea na mgomo. RFI / Carine Frenk
Matangazo ya kibiashara

Hata hivyo wito wao unatolewa wakati huu mwenyekiti wa baraza la magavana Josphat Nanok akitupilia mbali uwezekano wowote wa kufanyika mazungumzo kati yao na wauguzi waliokataa kurejea kazini.

Kwenye taarifa yake gavana Nanok ameagiza uongozi wa hospitali ambazo wauguzi wake hawajarejea kazini kuwafuta kazi baada ya mahakama ya kazi kusema kuwa mgomo huo ulikuwa batili.

Wauguzi wa hospitali nchini Kenya wamekuwa kwenye mgomo toka mwezi juni mwaka huu ambapo wanashinikiza kupewa nyongeza ya mshahara na kulipwa marupurupu yao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.