Habari RFI-Ki
Ushindi wa kenyatta wafutwa,Kenya kurejea katika uchaguzi ndani ya siku 60
Imechapishwa:
Cheza - 10:32
Mahakama ya Juu nchini Kenya imefuta ushindi wa rais Uhuru Kenyatta katika Uchaguzi uliofanyika tarehe 8 mwezi uliopita.Uamuzi huo ulitangazwa na Jaji Mkuu David Maraga jijini Nairobi Ijumaa asubuhi.Jaji Maranga alisema kuwa kati ya Majaji sita waliosikiliza kesi hiyo, wanne walifikia uamuzi kuwa Uchaguzi huo haukufanyika kwa mujibu wa Katiba ya sheria za Uchaguzi nchini humo.