Habari RFI-Ki
Raisi wa shirikisho wa soka barani Afrika ataka ushirikiano uimarishwe kati ya serikali na vyama vya soka
Imechapishwa:
Cheza - 09:33
Rais wa Shirikisho la soka barani Afrika Ahmad Ahmad anataka ushirikiano wa karibu kati ya serikali za bara Afrika na vyama vya soka kwa lengo la kuimarisha mchezo wa kandanda. Je, ushirikiano upi unahitajika kuwepo ? Inawezekana kweli ? Mataifa mengi ya Afrika yamekuwa yakiingilia uongozi wa vyama vya soka badala ya kusaidia kuinua soka mfano wa hivi karibuni ikiwa ni Sudan, na kusababisha Shirikisho la soka duniani FIFA kuyafungia kwa mujibu wa kanuni zake ambazo zinakataza serikali kuingilia uongozi wa soka. Je, ushirikiano huu unawezekana ?