Pata taarifa kuu
RWANDA-ISRAEL-USHIRIKIANO

Rais wa Rwanda azuru Israel

Rais wa Rwanda Paul Kagame ameanza ziara ya siku mbili nchini israeli ambako atakutana na rais wa nchi hiyo Reuven Rivlin Jumatatu hii Julai 10.

Rais wa Rwanda Paul Kagame madarakani toka mwaka 2000.
Rais wa Rwanda Paul Kagame madarakani toka mwaka 2000. REUTERS/Eric Vidal
Matangazo ya kibiashara

Kabla ya kukutana na mwenyeji wake, rais Kagame atakutana na waziri mkuu wa Israeli, Benjamin Netanyahu mjini Jerusalem.

Ziara ya rais Kagame inakuja mwaka mmoja baada ya waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuitembelea Rwanda julai 6 mwaka jana.

Mnamo mwezi Machi, rais wa Rwanda Paul Kagame alikua kiongozi wa kwanza barani Afrika kuhutubia kungamano kubwa la watu mjini Washington, nchini Marekani, ambao wanaiunga mkono serikali ya Israel, akisifu taifa hilo la Kiyahudi kuwa mfano kwa taifa lake kuzaliwa upya baada ya mauaji ya kimbari.

Rais Kagame alikuwa kiongozi wa waasi aliyezima na kumaliza mauaji ya Rwanda ya mwaka 1994 kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo ameliongoza taifa hilo toka mwaka 2000, wakati huu taifa lake likipona majeraha ya mauaji hayo na kuwa taifa la mfano kwenye ukanda wa nchi za Afrika Mashariki.

Rais Kagame alihudhuria mkutano wa mwaka kuhusu Israel na Marekani, ambapo amelisifu taifa hilo baada ya kufanikiwa kujiimarisha hata baada ya mauaji ya Holocaust na kuahidi Rwanda kuiunga mkono.

“Usalama wa raia ambao awali walilengwa kwa mashambulizi ili watokomee kamwe hauwezi kuwa wa kimwili tu,” alisema rais Kagame ambaye alishangiliwa na umati wa watu waliohudhuria kongamano hilo.

Nchi nyingi za Afrika zilikuwa zinaiona Israel kama muungaji mkono wa utawala wa kibaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, lakini katika miaka ya hivi karibuni Israel imeanza kurejesha uhusiano wa kawaida wa Kidiplomasia.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.