Pata taarifa kuu
KENYA-SOMALIA-AL SHABAB

Magaidi wa Al Shabab wazuiwa kuingia nchini Kenya

Polisi nchini Kenya wamefanikiwa kuwazuia magaidi sita wa Al Shabab kutoka nchini Somalia, waliokuwa wanapanga kuingia nchini humo kwa lengo la kutekeleza shambulizi la kigaidi.

Magaidi wa Al Shabab nchini Somalia
Magaidi wa Al Shabab nchini Somalia
Matangazo ya kibiashara

Inspekta Mkuu wa Polisi nchini humo Joseph Boinnet amesema washukiwa hao, wawili raia wa Kenya na wengine kutoka Somalia, walikuwa wametumwa na Kamanda wao kutoka kambi yao ya Burhanche.

Boinett amesema, maafisa wa usalama nchini Kenya walifanikiwa kuzuia shambulizi hilo kwa sababu ya ushirikiano wa karibu na wenzao wa Somalia mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mafanikio haya ya jeshi la Polisi nchini humo limekuja baada ya maafisa 20 wa Polisi kuuawa wiki kadhaa zilizopita Kaskazini mwa nchi hiyo baada ya magari waliyokuwa wanasafiria kukanyaga mabomu yaliyotegwa ardhini.

Kenya imeendelea kutishiwa usalama na kundi la Al Shabab baada ya kutuma wanajeshi wake nchini Somalia kupambana na kundi hilo mwaka 2011.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.