Pata taarifa kuu
KENYA-SOMALIA

Al Shabab yawauawa watu wawili Kaskazini Mashariki mwa Kenya

Watu wawili akiwemo afisa wa serikali wameuawa baada ya kushambuliwa na wanamgambo wa Al Shabab katika kaunti ya Mandera Kaskazini Mashariki mwa Kenya.

Wanamgambo wa Al Shabab nchini Somalia
Wanamgambo wa Al Shabab nchini Somalia i.onthe.io
Matangazo ya kibiashara

Maafisa nchini Kenya wanasema watu hao walitekwa kabla ya kuuawa na wanamgambo hao waliokimbilia nchini Somalia.

Polisi wamesema tayari maafisa wa usalama wametumwa katika eneo hilo kudhibiti usalama wakati huu msako mkali ukiendelea kuwatafuta magaidi hao.

Hii ndio mara ya kwanza ndani ya muda mrefu kwa ripoti za uvamizi wa Al Shabab kuripotiwa katika eneo hilo ambalo limekuwa chini ya ulinzi mkali.

Kundi la Al Shabab limeendelea kuwa hatari kwa serikali ya Kenya na usalama wa Afrika Mashariki.

Kenya ni miongoni mwa mataifa  ambayo yametuma vikosi vyake nchini Somalia chini ya mwavuli wa Umoja wa Afrika AMISOM tangu mwaka 2011 kupambana na Al Shabab.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.