Pata taarifa kuu
ICC-UGANDA-LRAC

Rais wa ICC atembelea watu walioteswa na LRA nchini Uganda

Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya ICC Jaji Silvia Fernandez de Gurmendi anazuru Kaskazini mwa Uganda, kukutana na waathiriwa walioteswa mikononi mwa waasi la Lords Resistance Army.

Majaji na makarani wa mahakama ya ICC, wakiwa wameketi wakati wa kesi ya Dominc Ongwen, 6 Desemba 2016
Majaji na makarani wa mahakama ya ICC, wakiwa wameketi wakati wa kesi ya Dominc Ongwen, 6 Desemba 2016 ICC media channel
Matangazo ya kibiashara

Waathiriwa hao wanasaidiwa kujikwamua kiuchumi na Shirika moja la Kimataifa linaloshirikiana na Mahakama ya ICC.

Ziara hii inakuja wakati huu Kamanda wa juu wa kundi la LRA Dominic Ongwen kesi yake ikiendelea katika Mahakama hiyo mjini Hague nchini Uholanzi.

Aliyekuwa kamanda wa kikosi cha waasi wa Uganda, LRA, Dominic Ongwen, akiwa katika mahakama ya ICC, 6 December 2016
Aliyekuwa kamanda wa kikosi cha waasi wa Uganda, LRA, Dominic Ongwen, akiwa katika mahakama ya ICC, 6 December 2016 ICC media outlet

Inaarifiwa kuwa kundi la LRA lilihusika na mabaya mengi nchini Uganda na katika nchi jirani, ikiwa ni pamoja na mauaji, ubakaji, uporaji, mateso kwa raia na watoto kutumiwa katika kundi hilo kama wapiganaji.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.