Watu 40 wapoteza maisha katika ajali ya boti nchini Tanzania
Watu arobaini walipoteza maisha katika ajali ya boti ambayo ilizama kaskazini mashariki mwa Tanzania. Boti ambayo iliku aikitokea katika bandari ya tanga ikielekea katika visiwa vya Pemba.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Boti hiyo ilikua imebeba watu 50 wakati ilipozama usiku wa Jumatatu kuamkia Jumanne hii Januari 10.
Miili kumi na mbili imepatikana na watu tisa waliokolewa, polisi imesema.
Boti hilo lilikua likielekea katika visiwa vya Pemba ikitokea katika bandari ya Tanga.
Sababu za ajali hiyo hazijajulikana kwa mujibu wa polisi.