UGANDA-SOMALIA-AMISOM
Askari wa Uganda wahukumiwa Somalia
Askari kumi na saba wa Uganda wa kikosi cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) wamesikilizwa Jumanne hii mbele ya mahakama ya kijeshi ya Uganda mjini Mogadishu.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Askari wanatuhumiwa kuuza vifaa vya kijeshi na mafuta katika mji mkuu wa Somalia.
Askari mmoja amekiri na amehukumiwa mwaka mmoja jela.
Hii ni mara ya kwanza mahakama ya kijeshi inajielekeza nchini Somalia kuwahukumu askari wa kikosi cha Umoja wa Afrika (AMISOM) kutoka Uganda tangu kutumwa kwa kikosi hiki miaka tisa iliyopita.
Uganda ni mchangiaji mkuu wa AMISOM, ambapo ina askari 22,000 nchi Somalia chini ya kivuli cha Umoja wa Afrika.