Pata taarifa kuu
Rwanda-Marekani

Serikali ya Marekani yaionya Rwanda kwa kuwanyima haki ya msingi wananchi wake

Serikali ya Marekani inaituhumu serikali ya Rwanda kuwakamata watu pasipo sababu na kuiomba serikali ya Kigali kuheshimu uhuru wa kujieleza, jambo ambalo limeilazimu serikali ya Rais Paul Kagame kujibu bila ya subira.

Ofisi ya wizara ya mambo ya nje ya Marekani
Ofisi ya wizara ya mambo ya nje ya Marekani
Matangazo ya kibiashara

Katika taarifa iliyosomwa na Marie Harf, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani, serikali ya rais Obama imeeleza wasiwasi wake kuhusu kutoweka kwa idadi kubwa ya watu katika mazingira tatanishi pamoja na vitisho vinavyoendelea dhidi ya waandishi wa habari.

Aidha, serikali ya Marekani inaiomba Rwanda kutoa maelezo kuhusu hatma ya raia wa rwanda waliokamatwa katika kipindi cha miezi miwili iliyopita na kuitaka iheshimu haki za binadamu kwa mujibu wa sheria za Rwanda na za kimataifa.

Onyo hilo limekuja saa chache baada ya kiongozi wa chama upinzani nchini Rwanda cha PS-Imberakuri Bernard Ntaganda kuachiwa huru ambapo ametumikia kifungo cha miaka minne jela kwa tuhuma za kujenga chuki, utengano na mifarakano nchini humo.

Akijibu tuhuma hizo za Marekani dhidi ya serikali, Louise Mukishiwabo Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda amewataka watu kuacha kutumia kila neno au tendo litakalowatia nguvu waasi wa kihutu wa FDLR pamoja na washirika wao na hivyo kuhatarisha maisha ya Wanyarwanda, na kwamba nchi yake haitasita kuchukua hatuwa madhubuti za kushughulikia tishio lolote kwa usalama wa Rwanda.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.