Pata taarifa kuu
UNHCR-WAKIMBIZI

UNHCR: Idadi ya wakimbizi yaongezeka na kufikia Milioni 65.6 duniani

Umoja wa Mataifa unasema idadi kubwa ya wakimbizi duniani imeongezeka na kufikia  Milioni 65.6 .

Wakimbizi wa Sudan Kusini wanaoishi nchini Uganda
Wakimbizi wa Sudan Kusini wanaoishi nchini Uganda REUTERS/Stringer/File photo
Matangazo ya kibiashara

Tume ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia wakimbizi inasema hili ni ongezeko la wakimbizi 300,000 ongezeko lililoshuhudiwa mwaka 2016.

Mkuu wa Tume hiyo Filippo Grandi amesema inasikitisha kuona idadi ya wakimbizi ikiendelea kuongezeka duniani kila wakati.

“Dunia inaonekana kushindwa kulinda amani,” amesema Bwana Grandi.

Soma pia makala haya:-Bonyeza

Aidha, amesema  asilimia 84 ya wakimbizi hao wanaishi katika mazingira magumu na ya umaskini.

Maeneo yaliyo na wakimbizi wengi ni kutoka barani Afrika, Mashariki ya Kati na barani Asia.

Nchi wanazotokea idadi kubwa ya wakimbizi:

  • Syria: Zaidi ya Milioni 5.5
  • Afghanistan: Milioni 2.5
  • Sudan Kusini: Milioni 1.4

Mataifa yepi yanaongoza kuwapa hifadhi wakimbizi ?

  • Uturuki : Milioni 2.9
  • Pakistan: Milioni 1.4
  • Lebanon: Milioni 1
  • Iran: 979,4000
  • Uganda: 940,800
  • Ethiopia: 791,600
Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.