Watano wapoteza maisha katika mlipuko Pangani Kenya
Takribani watu watano wamethibitika kupoteza maisha huku idadi ikihofiwa kuongezeka baada ya kutokea mlipuko uliojeruhi wengine 36 jumamosi nchini kenya.
Imechapishwa:
Bado ni muendelezo wa mashambulizi yasiyoeleweka nani anayehusika huku ikishuhudiwa watu 13 wakipoteza maisha tangu jumanne juma hili.
Mkuu wa polisi jijini Nairobi Benson Kibue amesema uchunguzi unafanyika kubaini ni aina gani ya bomu ilitumika kusababisha madhara yaliyojitokeza na ikiwa mshambuliaji alikuwa miongoni mwa abiria wa matatu hiyo au la.
Kwa mujibu wa polisi gari hiyo matatu hiyo ililipuka eneo la pangani baada ya kutoka eneo la jirani na nairobi isti lii eneo ambalo imejaa jamii ya wasomali.