Senzo Meyiwa auawa Afrika Kusini
2014 ulikua pia mwaka wa huzuni kwa wapenzi wa soka nchini Afrika Kusini baada ya kuuawa kwa nahodha wa Bafana Bafana kipa Senzo Meyiwa.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Mwezi Oktoba, Meyiwa alipigwa risasi na watu waliojihami kwa silaha jijini Johannersburg akiwa na mpenzi wake.
Meyiwa aliisaidia Afrika Kusini kufuzu katika michuano ya Mataifa bingwa mwaka ujao nchini Equitorial Guinea.
Mbali na Meyiwa, kifo cha mchezaji mwingine kilichogusa wapenzi wa soka ni mchezaji wa klabu ya JS Kabylie ya Algeria, Mcameroon Albert Ebossé aliyepigiwa na kitu kizito kichwani na mashabiki wa wa JS Kabylie, baada ya klabu hiyo kupoteza mabao 2 kwa 1 dhidi ya USM Alger.