BANGLADESH-HAKI
Bangladesh: Watu 16 wahukumiwa kifo kwa mauaji ya msichana mdogo aliyechomwa akiwa hai
Mahakama ya Bangladesh leo Alhamisi imewahukumu kifo watu 16 kwa mauaji ya msichana wa miaka 19 aliyechomwa moto akiwa hai baada ya kkufikisha malalamiko yake mahakamani kuwa alibwakwa na mkuu wa shule ya kidini (madrasa).
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kifo cha Nusrat Jahan Rafi kilichotokea mnamo mwezi Aprili kilihuzunisha wengi na kusababisha kuzuka kwa maandamano makubwa katika taifa hili la Asia Kusini.
Washtakiwa 16, pamoja na mwalimu wa msichana huyo na wenzake watatu, walihukumiwa tangu Juni na Mahakama Maalum katika Wilaya ya Feni (kusini-mashariki).