Pata taarifa kuu
IRAN-JAPAN

Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe ziarani Iran

Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe anafanya ziara nchini Iran, ziara inayokuja wakati huu taifa hilo likiwa kwenye mvutano mkubwa na utawala wa Washington.

Waziri mkuu wa Japan, Shinzo Abe.
Waziri mkuu wa Japan, Shinzo Abe. AFP PHOTO/Ludovic Marin
Matangazo ya kibiashara

Hii ni ziara ya kwanza ya waziri mkuu wa Japan nchini Iran katika kipindi cha miaka 41.

Akiwa mjini Tehran waziri mkuu Abe atakuwa na mazungumzo na mwenyeji wake rais Hassan Rouhani.

Nchi ya Iran imekuwa katika mzozo na Marekani tangu rais Donald Trump atangaze kujiondoa kwenye mkataba wa kimataifa wa Nyuklia na nchi ya Iran mwezi Mei mwaka jana.

Tangu ilipojiondoa, Marekani imetangaza vikwazo zaidi vya kiuchumi dhidi ya Iran, vikwazo ambavyo vimesababisha Japan isitishe ununuaji wa mafuta ya Iran kama sehemu ya kutekeleza onyo la vikwazo vya Marekani.

Marekani katika makataa yake imeyataka mataifa na makampuni kusitisha ununuaji wa mafuta ya Iran, ikisema nchi itakayoenda kinyme itakumbana na vikwazo vya nchi yake.

Kwa upande wake Iran imejibu kwa kutishia kuanza upya urutubishaji wa Urani ikiwa mataifa ya magharibi yaliyosalia kwenye mkataba wa sasa hayatailinda.

Licha ya uwepo wa taarifa kuwa waziri mkuu Abe ameenda Tehran akiwa na ujumbe wa utawala wa Washington, ofisi yake imekanusha madai hayo ikisema ziara ya Abe ni ziara ya kawaida.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.