Pata taarifa kuu
INDONESIA-MAUAJI-TSUNAMI

Tsunami yauwa watu 168 nchini Indonesia

Watu zaidi ya 160 wamepoteza maisha na karibu 600 wamejeruhiwa katika mji wa Sunda Strait nchini Insdonesia, baada ya kutokea kwa Tsunami katika mji huo wa Pwani.

Mlipuko wa Volkano nchini Indonesia
Mlipuko wa Volkano nchini Indonesia Phys.org
Matangazo ya kibiashara

Mbali na mauaji hayo, watu zaidi ya 20 bado hawajapatikana lakini pia mamia ya majengo yameharibika.

Maafisa wanasema kuwa, watu wengine zaidi ya 500 wamejeruhiwa na wanaendelea kupata matibabu.

Kuna hofu kuwa, idadi ya vifo huenda itaendelea kuongezeka.

Watalaam wanasema kuwa chanzo cha janga hilo ni maporomoko ya ardhi, chini ya bahari baada ya kulipuka kwa volkano hivi karibuni.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.