Pata taarifa kuu
KOREA KASKAZINI-KOREA KUSINI

Kim Jong Un ataka kuandika historia ya kumaliza mvutano na Korea Kusini

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amekutana na ujumbe kutoka Korea Kusini na kusema lengo lake ni kufanikisha mazungumzo kati ya nchi hizo mbili.

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un akisaliamiana na Mjumbe wa Korea Kusini Chung Eui-yong, jijini Pyonyang Machi 05 2018
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un akisaliamiana na Mjumbe wa Korea Kusini Chung Eui-yong, jijini Pyonyang Machi 05 2018 The Presidential Blue House/Yonhap via REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Kim Jong-un amesema anataka kuacha historia ya kuunganisha Korea Kaskazini na Korea Kusini na kumaliza wasiwasi wa kiusalama dhidi ya jirani yake kutokana na mradi wake wa nyuklia.

Kingozi huyo amekutana na ujumbe wa Korea Kusini na kula nao chakula cha jioni, kikiwa ni kikao cha kwanza kati ya ujumbe wa Seoul na kiongozi huyo wa Pyongyang tangu alipoingia madarakani mwaka 2011.

Uhusiano kati ya nchi hizi mbili umeonekana umeanza kuimarika tangu michezo ya Olimpiki ya msimu wa baridi iliyofanyika nchini Korea Kusini.

Kabla ya kuanza kwa michezo hiyo, Korea Kusini ilikubali kuja kwa wachezaji wa Korea Kaskazini katika michezo hiyo na hata kuunda timu moja ya mchezo wa magongo.

Mkutano huu umetoa matumaini ya kuendelea kufanyika kwa mazungumzo zaidi katika siku zijazo ili kuondoa wasiwasi wa kiusalama kati ya Pyongyang na Seoul.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.