Pata taarifa kuu
KOREA KASKAZINI-UNSC-USALAMA

Korea Kaskazini: Tutaendelea kutengeneza silaha za nyuklia

Nchi ya Korea Kaskazini hii leo imesisitiza kuwa itaendelea na mradi wake wa kutengeneza silaha za nyuklia kama majibu ya kile ilichosema ni vikwazo ilivyowekewa na baraza la usalama la umoja wa Mataifa.

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un akiahidi kuendelea na mpango wake wa kutengeneza silaha za nyukilia na kurusha mkombora ya masafa marefu.
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un akiahidi kuendelea na mpango wake wa kutengeneza silaha za nyukilia na kurusha mkombora ya masafa marefu. KCNA/ via REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Akizungumza jijini New York Marekani balozi wa Korea Kaskazini kwenye umoja huo Han Tae Song amesema kilichofanywa na baraza la usalama hakitaacha kipite kwakuwa umoja huo umedhamiria kuiumiza nchi yake.

Kwa upande wake rais wa Marekani Donald Trump amesema vikwazo hivi licha ya kuwa havitakuwa na athari kubwa sana kwa Korea Kaskazini lakini vinatuma ujumbe kuwa dunia imechoshwa na kejeli za Pyongyang.

Vikwazo hivi vimechukuliwa baada ya juma moja lililopita utawala wa Pyongyang kufanya jaribio kubwa zaidi la silaha ya nyuklia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.