Zoezi la kutafuta mabaki ya ndege iliotoweka laendelea Indonesia
Waokoaji wanakwenda Mashariki mwa Indonesia kutafuta mabaki ya ndege ya abiria iliyokuwa na abiria 54 kutoweka siku ya Jumapili mwishoni mwa juma lililopita.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Hatua hii inakuja baada ya kuonekana kwa vipande vya ndege hiyo iliyopoteza mawasiliano ikitokea mjini Jayapura katika mkoa wa Papua.
Ripoti zinasema ndege hiyo ilikuwa na abiria 44 watu wazima na watoto watano na juhudi za kutafuta miili na mabaki ya ndege hiyo zinaendelea.
Inaripotiwa kuwa ndege hiyo ilionekana ikianguka katika Mlima mmoja karibu na eneo la Oksibil.
Kiongozi wa kikosi cha uokoaji Bambang Soelistyo, amesema kuwa moshi ulionekana ukifuka katika eneo hilo.
Hii ndio ajali ya hivi karibuni kutokea barani Asia.