Marekani: Makubaliano yafikiwa kuhusu bajeti, kuelekea kufadhili ujenzi wa ukuta
Marekani inapanga kuepuka kukwama tena kwa shughuli za serikali. Bunge la Wawakilishi limepitisha muswada wa fedha ambao tayari umeidhinishwa na Bunge la Seneti.
Imechapishwa:
Ikulu ya White House inatarajia kutia saini kwenye sheria ya bajeti hata kama nakala hiyo haizungumzii dola Bilioni 5.7 ambayo rais anahitaji kwa ujenzi wa ukuta kwenye mpaka na Mexico.
Ili kupata fedha anazohitaji, rais Donald Trump anatarajia kutangaza hali ya dharura kwenye mpaka wa Marekani na Mexico. Hatua ambayo itamuwezesha kutopingwa na Bunge la Wawakilishi.
Muswada wa kifedha ulipitishwa Alhamisi wiki hii na idadi kubwa ya wajumbe wengi katika bunge la Seneti, linalodhibitiwa na chama cha Republican, na Bunge la Wawakilishi, lililoongozwa idadi kubwa ya wabunge kutoka chama cha Democratic, baada ya mjadala mkali. Muswada huo ulipitishwa na wabunge 300 dhidi ya 128 walioupinga.
"Rais atasaini muswada wa kifedha, lakini wakati huo huo atatangaza la hali ya dharura na nikamwambia kuwa nitaunga mkono hatua hiyo ya dharura, "amesema Seneta Mitch Mc Connell.
When the Senate votes on the agreement to fund the government, we’ll be voting to avoid a second partial shutdown and provide the certainty of a fully-functioning federal government.
Leader McConnell (@senatemajldr) February 14, 2019
Hata hivyo awali wabunge wengi na maseneta kutoka chama cha Republican walitangaza kwamba watapinga tangoze lolote la Trump kuhusu hali ya dharura kwenye mpaka wa Marekani na Mexico, kwa mujibu wa mwandishi wetu Washington, Anne Corpet.
Kwa upande wa kiongozi mkuu wa wabunge wa chama cha Democratic Nancy Pelosi, amesema ni matumizi tu mabaya ya madaraka kwa Rais Trump. "Kwanza, hakuna hali ya dharura kwenye mpaka, kuna changamoto ya kibinadamu tunayokabiliana nayo. Lakini mbali na hilo rais anajaribu kuzua jambo ambalo halitakiwi kutumiwa kwa sasa, amesema Nancy Pelosi.
Declaring a national emergency would be a lawless act, a gross abuse of the power of the presidency and a desperate attempt to distract from the fact that @realDonaldTrump broke his core promise to have Mexico pay for his wall.
Nancy Pelosi (@SpeakerPelosi) February 14, 2019